Thursday, January 10, 2013

PICHA : JK AWATEMBELEA WANACHAMA UVCCM, KATIKA CHUO CHA TABORA




PICHA : TUNAWASILISHA MAONI

 
Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Bw. Absolom Kibanda akimkabidhi maoni ya Jukwaa hilo kuhusu katiba Mpya Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Prof. Mwesiga Baregu katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam leo  

Mwanachama wa Jukwaa la Wahariri (TEF) Bw. Deodatus Balile akiwasilisha maoni ya Jukwaa hilo kuhusu Katiba Mpya katika mkutano uliofanyika katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam leo. Wengine ni Bw. Ruge Mutahaba (kushoto) kutoka Clouds Media Group na Bw. Yasin Sadik kutoka gazeti la Hoja.


Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Bw. Kajubi Mukajanga akiwasilisha maoni ya Baraza hilo kuhusu Katiba Mpya katika mkutano uliofanyika katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Bi. Pili Mtambalike kutoka MCT.


Saturday, December 15, 2012

WAAJIRI BORA WAPATIWA TUZO

Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akimkabidhi Mkurugenzi wa Rasilimali  Watu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),Kenneth Wanyoto cheti baada y kuwa mmoja wa wafadhiri wa hafla ya kuwazawadia waajiri Bora wa Mwaka 2012 katika hafla  iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.Kushoto ni Mwenyekiti wa ATE, Almas Maige


Mkurugenzi wa Rasilimali  Watu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),Kenneth Wanyoto akishangilia baada ya Rais Jakaya Kikwete kumkabidhi tuzo ya ushindi wa tatu ya Mwajiri Bora wa Mwaka 2012 katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.



Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akimkabidhi Mkurugenzi wa  Rasilimali  Watu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),Kenneth Wanyoto cheti baada y kuwa mmoja wa wafadhiri wa hafla ya kuwazawadia waajiri Bora wa Mwaka 2012 katika hafla  iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.Kushoto ni Mwenyekiti wa ATE, Almas Maige



Wanyoto akipita na tuzo mbele ya Rais Kikwete pamoja na Mwenyekiti wa ATE, Almas Maige

TAARIFA KUTOKA IKULU




Rais wa Madagascar, Mheshimiwa Andry Rajoelina ambaye amewasili mjini Dar es Salaam mchana jana Ijumaa, Desemba 14 kwa ziara ya kikazi ya siku mbili nchini akiwa  na mwenyeji wake,  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Ikulu, tayari kuanza mazungumzo rasmi.

Rais Kikwete ni Mwenyekiti wa Tume ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambapo amepewa jukumu na viongozi wenzake ndani ya Jumuiya hiyo kukutana na viongozi wa Madagascar kuwaelezea maamuzi ya mkutano wa viongozi hao wa SADC uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Dar Es Salaam.Kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Ikulu, Dar Es Salaam, mwanzoni mwa wiki hii, Mheshimiwa Ravalomanana alithibitisha kuwa amekubaliana na maamuzi ya viongozi wa SADC.

Miongoni mwa mambo mengine, viongozi hao wa SADC wanataka viongozi hao wawili wa Madagascar washawishiwe na wakubali kutogombea katika Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika nchini humo mwakani.