Saturday, December 15, 2012

WAAJIRI BORA WAPATIWA TUZO

Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akimkabidhi Mkurugenzi wa Rasilimali  Watu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),Kenneth Wanyoto cheti baada y kuwa mmoja wa wafadhiri wa hafla ya kuwazawadia waajiri Bora wa Mwaka 2012 katika hafla  iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.Kushoto ni Mwenyekiti wa ATE, Almas Maige


Mkurugenzi wa Rasilimali  Watu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),Kenneth Wanyoto akishangilia baada ya Rais Jakaya Kikwete kumkabidhi tuzo ya ushindi wa tatu ya Mwajiri Bora wa Mwaka 2012 katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.



Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akimkabidhi Mkurugenzi wa  Rasilimali  Watu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),Kenneth Wanyoto cheti baada y kuwa mmoja wa wafadhiri wa hafla ya kuwazawadia waajiri Bora wa Mwaka 2012 katika hafla  iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.Kushoto ni Mwenyekiti wa ATE, Almas Maige



Wanyoto akipita na tuzo mbele ya Rais Kikwete pamoja na Mwenyekiti wa ATE, Almas Maige

TAARIFA KUTOKA IKULU




Rais wa Madagascar, Mheshimiwa Andry Rajoelina ambaye amewasili mjini Dar es Salaam mchana jana Ijumaa, Desemba 14 kwa ziara ya kikazi ya siku mbili nchini akiwa  na mwenyeji wake,  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Ikulu, tayari kuanza mazungumzo rasmi.

Rais Kikwete ni Mwenyekiti wa Tume ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambapo amepewa jukumu na viongozi wenzake ndani ya Jumuiya hiyo kukutana na viongozi wa Madagascar kuwaelezea maamuzi ya mkutano wa viongozi hao wa SADC uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Dar Es Salaam.Kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Ikulu, Dar Es Salaam, mwanzoni mwa wiki hii, Mheshimiwa Ravalomanana alithibitisha kuwa amekubaliana na maamuzi ya viongozi wa SADC.

Miongoni mwa mambo mengine, viongozi hao wa SADC wanataka viongozi hao wawili wa Madagascar washawishiwe na wakubali kutogombea katika Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika nchini humo mwakani.

Tuesday, December 11, 2012

HONGERA ZANZIBAR HEROES - Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

 Mashabiki wa Timu ya Zanzibar, Zanziabar Heroes, wakiilaki Timu yao.
 Kikosi Cha Timu ya Zanzibar, Zanzibar Heroes
 Nahodha wa timu ya Zanzibar Hereos Nadir Haroub Kanavaro akiishukuru Serekali ya Zanzibar kwa mashirikiano iliyotoa kwa timu hiyo.

Naibu Waziri wa Habari,Utamadu Utamaduni na Michezo Bi Hindi Hamadi akiwashukuru wa wachezaji pamoja na viongozi wao kwa ushindi walio upata wa nafasi ya tatu katika mashindano ya Challenge Uganda.
                                                     ************************


NA HABARI MAELEZO, ZANZIBAR

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema imefurahishwa sana na kiwango cha mchezo kilichooneshwa na Timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) katika Mashindano ya Challenge licha ya kuambulia mshindi wa tatu wa mashindano hayo.
                                    
Aidha katika kuipongeza Timu hiyo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein amepanga kukutana na Vijana hao ikiwa ni pamoja na kubadilishana mawazo ya kuimarisha kikosi cha Timu hiyo.
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Bihindi Hamad Khamis ameyasema hayo ukumbi wa Hoteli ya Bwawani wakati alipokuwa akizungumza na Timu hiyo mara baada ya kuwasili Zanzibar kutoka Uganda.

"Naleta salamu Rasmi za Serikali kwa juhudi kubwa mliyoifanya kule Uganda na Rais kasema atapanga siku ya kukutana nanyinyi ili mbadilishane naye mawazo ya kuboresha timu zaidi" alisema Bihidi.

Amesema juhudi ambazo zilioneshwa na Vijana wa Zanzibar Heroes zinafaa kuthaminiwa kutokana na kucheza na timu ziliozojaa uzoefu na wachezaji maarufu lakini vijana hao walipigana kiume na kuambulia nafasi ya tatu.

Bihindi amewataka Wachezaji wa Zanzibar Heroes kutunza afya na kuimarisha mazoezi yao ili michuano ya mwakani waweze kuwaletea Wazanzibar kikombe cha Ushindi wa Mashindano hayo.

Ameongeza kuwa kiwango cha mchezo walichoonesha vijana hao kiliwasisimua Wazanzibari wengi na kuwasababisha kutenga muda wao kwa ajili ya kuangalia timu yao kila ilipokuwa ikicheza.

Aidha aliwataka Wachezaji hao kuitumia fursa ya kuonana na Rais kuelezea mipango wanayodhani itakuwa bora katika kuimarisha Timu hiyo kwa faida yao na Taifa kwa ujumla.
Kwa upende wake Meneja wa Timu ya Zanibar Heroes Salim Msabah ameiomba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kushirikiana bega kwa bega na Chama cha Soka Zanzibar ZFA katika kuhakikisha timu inapatiwa maandalizi ya mapema ndani na nje ya Nchi ili kuimarisha kikosi cha timu hiyo.
Amesema anaamini Zanzibar kuna vipaji vya kutosha katika fani ya Soka na hivyo kinachohitajika ni namna bora ya kuviendeleza vipaji hiyo ikiwa ni pamoja na maandalizi ya mapema.

Nahodha wa Timu hiyo Nadir Haroub amesema lengo lao lilikuwa kutwaa Ubingwa wa Michuano hiyo lakini nafasi waliyoipata ya Mshindi wa tatu imewafariji kutokana na kuifunga timu pinzani kwao.

Amedai kuwa ushindi huo pia utawajengea heshima wale wachezaji wa Zanzibar wanaocheza Soka katika ligi ya Bara kutokana na kuifunga Kilimanjaro Stars ambayo wanacheza wake wanacheza wote katika ligi hiyo.

Timu ya Zanzibar Heroes iliibuka Mshindi wa Tatu wa Mashindano ya Challenge yaliyofanyika nchini Uganda baada ya kuichapa Kilimanjaro Stars kwa mikwaju ya Penalti 6-5 na kufanikiwa kupata zawadi ya kitita cha Dola za Marekani 10,000.